PATA HABARI KAMILI YA MAZISHI WA WALIOKUFA KUTOKANA NA MLIPUKO WA BOMU OLASITI ARUSHA

0
Leo ilikuwa nisiku nyingine ya majonzi ambapo maelfu ya watu walijitokeza wakiwa na nyuso za huzuni na majonzi tele kuwapumzisha ndugu zetu waliotangulia mbele ya haki kutokana na mlipuko wa bomu uliotokea jpili iliyopita ambapo mpaka sasa watu watatu wameshafariki na ndo hao leo wamezikwa kwa heshima kubwa mbele ya kanisa la katoliki huko olasiti.. 
Waliokumbwa na mauti kutokana na mlipuko wa bomu hilo ni Mama Reginald loning'o laizer  aliyezaliwa mwaka 1963 mkazi wa olasiti ambaye ameacha mume na watoto saba.
JAMESGABRIEL KESSY aliyezaliwa Majengo Arusha mwaka 1997 aliyekuwa mwanafunzi wa kidato cha pili shule ya sekondari ya Arusha Day. amewacha wazazi wke na watoto wenzake watatu.
PATRICIA JOACHIM ASSEY aliyezaliwa Majengo Arusha mwaka 2003.ameacha wazazi wake ambapo mama yake mzazi amelazwa Hospitali ya Muhimbili akipata matibabu zaidi baada ya kujeruhiwa na bomu siku hiyo..

KIPEPERUSHI CHENYE PICHA ZA MAREHEMU WOTE NA WASIFU WAO..

Ifuatayo ni habari fupi pamoja na picha ya yale yote yaliyotokea katika mazishi hayo.
1-Watu walifika kanisani tayari kabisa kwaajili ya kupokea miili ya marehemuu 
2-Kuingia kwa wageni rasmi
   WAGENI RASMI WALIOHUDHURIA NI 
1.Waziri mkuu Mizengo Pinda
2.waziri mkuu mstaafu mh. Edward lowassa
3.Waziri nchimbi
4.Mwenyekiti wa CHADEMA ndugu Freeman Mbowe
5.Mwenyekiti Wa NCCR-MAGEUZI ndugu JAMES  MBATIA
5.Mkuu wa mkoa wa arusha ndugu mulongo
6.Mbunge wa Arusha mh. Godbless Lema
7.Viongozi kutoka serikali ya Zanzibar
8.Wabunge mbalimbali
9.viongozi wa dini mbali mbali akiwami shekhe mkuu wa Arusha,Viongozi wa dini ya kihindu
10.pamoja na viongozi mbalimbali wa usalama wa Taifa
3-Miili ya marehemu kufika kanisani na kuingizwa kanisani ambapo kwaheshima kubwa kabisa miili yote iliingizwa na viongozi wa katoliki.
4-Baada ya miili kuingizwa Kanisani Misa ya Kubariki kanisa jipya ilianza ikiwanipamoja na kunyunyuzia maji ya baraka.
4-Ilifanyika ibadamaalum ya kuwapokea Marehemu wote watatu ndani ya kanisa.
5-kwaya nayo ilipewa nafasi ya kuimba
6-kisha ibada baada ya ibada Baba Askofu Mkuu wa  Jimbo la Arusha la Kanisa Katoliki jijini Arusha Muadhama Josephat  Lebulu alikaribiswa kutoa neno ambapo alianza kwa kuwashukuru watu wote
7- Baada ya neno kutoka kwa askofu mkuu wa Jimbo la arusha watu waliungana kutoa Sadaka.
8-Kilichofuatia ilikuwa nikusomwa kwa wasifu wa marehemu wote Mama Regina,Patricia na James.
9-Kisha Ulifika wakati wa salamu za rambirambi kutoka kwa viongozi mbalimbali wa dini na waserikali.
   Wakwanza kutoa salamu za rambirambi alikuwa ni ndugu Ngalale Kumtwa ambaye ni kiongozi wa baraza la Maaskofu. kama ilivyo alianza kwakutoa pole kwa wafiwa wote kisha alinza kulalamikia vitendo viovu hasa vya kidini dhidi ya Wakristo hapa Tanzania, aliendelea kuelezea kuwa kwasasa mahusiano baina ya Waislamu na Wakristo unazidi kuzorota pia aligusia na kuelezea kuhusu mkutano mkubwa wa baadhi ya waislamu ambao ulifanyika Daresalam katika ukumbi wa Diamond Jubilee uliofanyika mwaka 2011 ambapo waislamu walidai kuwa serikali inawapendelea sana wakristo, alizidi kuelezea kuwa baadhi ya waislamu hao waliafikia kufa ama kuua kwaajili ya kueneza uislamu na kuungamiza ukristo hapa Tanzania. Pia aliilamu sana serikali kushindwa kukemea nakudhibiti matukio hayo.. Aliomba vyombo vya dola kuchimba ndani zaidi na kuwafahamu wahusika wote wanaoeneza vita hivi vya udini na kuwakamata kisha kuwafikisha mbele ya sheria..
      Wapili alikuwa ni Baba Askofu drAlex Malasusa kama ilivokawaida naye alianza kwakutoa pole kisha aliwawafariji wafiwa wote na kuwapa moyo kwa kuwaambia ya kuwa risasi,mabomu na uchomaji wa makanisa visitukatishe tamaa wakristo kwani ukristo upo katika mioyo yetu alizidi kusema kuwa siku ya mwisho hatutihukumiwa kwa mabaya tuu bali tutahukumiwa kwa yale mema ambayo hatukuyatenda hapa duniani.
        Salamu za  tatu za rambirambi zilitoka kwa UMOJA YA MADHEHEBU ARUSHA ambapo mjumbe alitoa pole na pia alisema kuwa jambazi hana ndugu na nchi hii niya watu wote na hakuna dini yenye chama.
         Salamu za nnezilikuwa zitoke kwa shekhe mkuu wa BAKWATA ila aliondoka baada ya ibada kwani alienda sehemu nyingine kwaajili yamaziko mengine.
          Salamu Ya tano na mwisho kabisa ilitoka kwa MH. Mizego Pinda ambaye niwaziri mkuu wa Tanzania aliyetoa salamu kwaniaba ya serikali na viongozi wote.. Kama ilivyoalianza kwakutoa salamu zake za pole kwa wafiwa wote na Watanzania wote kwaujumla..Neno kubwa la waziri mkuu nikuwa hakuna aliyetarajia mauti ila ndo hivyo mauti yamewakumba marehemu hao kwahiyo nilazima tukubaliane na hilo na tuwaombee ili walazwe mahali pema peponi pia waziri mkuu hakuishia hapo alisemma ya kuwa kuua mkristo mmoja au kiongozi mmoja sio kukomesha ukristo, ukristo na uislamu unahistoria kubwa sana na utakuwa unajidanganya kuwa ukiua mufti mmoja utakuwa umeua uislam. Dini hizi zote mbili zina nguzo ndefu sana.. Katika kumalizia waziri mkuu alitoa msimamo waserikali kwa kusema kuwa serikali itapambana na kukomesha kundi hilo linalosababisha vita vya kidini nchini.Pia ameamrisha ofisi ya mambo ya ndani kufanya kazi ya ziada kukomesha uhalifu huu na aliwaomba wananchi wote wasaidiane na polisi kutoa taarifa juu ya wahalifu wote na serikali itawakamata na kuwafikisha mbele ya sheria..  Katila  kumalizia waziri mkuu alimalizia kwa kutaja kiasi cha rambirambi alichokabidhiwa ambapo nijumla ya milioni 12,kumi zikitoka benki ya NMB namillioni mbili zilitoka kwabbadhi ya viongozi ambao alifanya nao kikao cha serikali ya vitongoji ambao wao binafsi walijichanga hapohapo na kupatikana kwahizo milioni mbili..pia ofisi ya waziri mkuu ilitoa sh.millioni mia 100,000,000 pia serikali itagharamikia matibabu yote na hata ikitokea majeruhi akahitaji matibabu nje ya nchi serikali itagharamikia mataibabu hayo..
10-Baada ya salamu za rambirambi ilifuatia nenpo la shukrani ambalo lilitolewa na Askofu Mkuu Lebulu.alianza kwa kutoa pole kisha alitoa shukrani kwa watu wote wakiwamo viongozi wote wadini na serikali,viongozi ya serikali ya Zanzibar waliofunga safari hadi katika eneo latukio,hospitalini nasiku ya mazishi pia,viongozi wa BAKWATA uliowawakilisha waislamu wote Tanzania,viongozi wa dini ya Wahindu na viongozi wote wadini wanao thamini na kujali utu wa binadamu pia alitoa shukrani kwa wanaOlasiti wote,WanaArusha,Waaumini wote na Watanzania kwa ujumala walishiriki kwa hali na mali katika tukio hili tokea siku ya mlipuko hadi leo hii..
11-Mwisho kabisa ilikuwa ni shughuli nzima ya kwenda kuwapumzisha salama ndugu zetu wote waliotutoka kutokana na mlipuko wa bomu..
ZIFUATAZO NI BAADHI YA PICHA ZIKIONESHA TUKIO ZIMA ILIVYOKUWA..
 MAGARI ZILIZOBEBA MIILI YA MAREHEMU IKIWASILIA NJE YA KANISA
WAZIRI MKUU MSTAAFU MH.EDWARD LOWASSA AKIWASILI KANISANI
 MH. JAMES MBATIA AKIWASILIA KANISANI

MAPADRI WAKIJIANDA TAYARI KABISA KWAAJILI YA KUBEBA MAJENEZA YENYE MIILI YA MAREHEMU WOTE







 PICHA ZIKIONESHA UMATI WAWATU WALIOFIKA KUJA KUZIKA
 MUONEKANO WA KANISA KWA NDANI

 ENEO BOMU LILIPOTUA



 WAZIRI NCHIMBI AKIWASILIA
 MAJENEZA YALIYOBEBA MAREHEMU WOTE YAKIWA NDANI YA KANISA

0 comments: